Monday, January 31, 2011

Kuna haja ya wasomi kubadilika katika hili

Na Kagusa Manjemu

Kadiri uelewa kuhusu mazingira safi unavyohitajika duniani ndivyo wasomi wanavyoogoza kwa kutojali mazingira yanayowalea. Chukulia mfano nyuklia na taka za viwandani zikiwamo sumu na moshi vitokanavyo na michakato ya kutenenezea bidhaa mbalimbali, vyote ni matokeo ya wasomi na harakati zao za maendeleo kisayansi na kiuchumi pia. Mnamo karne ya kumi na moja, si shahada ya Baolojia,Kemia au Fizikia iliyokuwapo, lakini si ukame wala ongezeko la hali joto lililowahi kuikumba Dunia...
Zifuatazo ni picha ambazo zinaonyesha uzembe dhidi ya utunzaji wa mazingira miongoni mwa wanafunzi wa Chuo kikuu kishiriki cha Tumaini Iringa.....


Kopo la kutupia taka likiwa na taka chache  pamoja na sababu kuwa kuna uhaba wa makopo haya

Sehemu isiy rasmi kwa taka ikiwa imesheheni makopo na taka nyingine





Eneo lenye mikusanyiko ya watu wengi kama hili la Cafe Hall, hakuna hata kopo moja la kutupia taka


Nani anayehusika na taka hizi zilizopo sehemu ambayo si sahihi?
Wasomi kubadilika ni lazima kwa sasa.. hakuna faida yoyote kimsingi itakayopatikana kwa wewe kuchafua mazingira unayoishi...

7th Inter-Universities Competition in Nairobi

Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Tumaini Iringa akishangilia ushindi wa mpira wa miguu dhidi ya Naazarene University. Tumaini ilishinda 2-1 katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Kenyata University.



Mkuu wa chuo cha Tumaini-Iringa, Prof N.T Bangu (katikati mwenye suti nyeusi) akiwa na timu ya michezo ya chuo hicho kabla ya kuondoka kwenda Nairobi kwenye mashindano ya vyuo vikuu vya Africa Mashariki


Kila Chuo kilikuwa na namna yake ya kushangilia



Moja ya jengo la chuo kikuu Kenyata-Kenya 

Timi mpira wa kikapu ya chuo kikuu Tumaini wakiwa mazoezini Naorobi
Kitambo kidogo kabla ya kuingia uwanjani
Kuuza sura kama kwaida
Mdogomdogo kamaa!!!!!!! Ulaya
Daaaa!!!!!! so tired bro.
TUICo football team
Nairobi-Kenya
Ushindi ni jadi yetu
Kazi na dawa chief Lwanji


Timu ya mpira wa kikapu ya wanawake katika mazoezi kabla ya kuingia uwanjani











Friday, January 28, 2011

News in Picture

Tumaini University welcome first year's ceremony

Hivi ndivyo mambo  yalivyokuwa

Usanii katika Sanaa ya Filamu


Emmanuel Myamba,
Mmoja wa wasanii wa filamu nchini Tanzania 

Na Sango Shabani
Ni furaha ya kila Mtanzania  hasa yule mpenzi wa filamu za kibongo, kwani tasnia hii imefanikiwa kupiga hatua  na kuweza kujulikana ndani na nje ya Tanzania. Maendeleo haya yameanza kushusha manunuzi ya filamu toka Nigeria ambazo kwa kipindi kirefu yalikuwa yametawala katika soko la hapa nchini.
Tunawapongeza wale wachache wenye moyo wa kujitolea ambao wameifikisha tasnia hii hapa ilipo. Pamoja na  mafanikio tuliyofikia,  lakini bado kuna mapungufu kwenye filamu zetu ambayo kama yatarekebishwa, tasnia hii itaweza kufika mbali zaidi  na kuleta changamoto ndani na nje ya Afrika.
Nchi yetu imebahatika kuwa  na watu wenye vipaji vya kuigiza na kuuvaa uhusika ipasavyo. Ni mambo machache yanayo yanayoifanya tasnia hii kupoteza dira  na kupewa jina la “ usanii katika sanaa ya filamu”. Hii ni sababu ya mapungufu yanayoonekana dhahiri  kwenye filamu zao.
Kama ilivyo kawaida kwenye kila kilicho na mafanikio lazima kuwepo watu wenye upeo wa tofautii hasa kukwamisha suala zima la mafanikio. Hili ndio kichocheo kikubwa kinachokwamisha tasnia hii ya filamu . Wasanii wamekuwa wakilalamikia watu wa cable, yaani watu wanaofikishia watu mawimbi ya stesheni kadhaa za televisheni.
“Ikitokea mtu  mmoja kati  ya wale waliounganishwa na  cable akaweka CD ya filamu  ya kibongo au yeyote  lakini kwa  kuwa  tunaongelea filamu za kibongo  wanaweza kuona watu zaidi ya laki saba mwisho wa siku  CD ,DVD ama VHS zinakosa  wanunuzi sokoni” mmoja wa wadau wa tasnia ya filamu akitoa dukuduku lake kwenye kituo kimoja cha televisheni nchini.

Tatizo kubwa linalosababisha tasnia hii ipoteze uhalisia ni suala la mavazii hasa kwa waigizaji wa kike. Kumekuwa na upotoshwaji wa uhalisia kwenye mavazi. Watu wamekuwa wakishindwa kutofautisha mavazi kati ya  mshichana anayeuza mwili na yule mwenye heshima zake. Ni jambo la kawaida katika  filamu zetu  kumuona msichana akiwa kazini lakini nguo zake zikiwa za starehe .
Tatizo lingine liko kwenye suala la uhalisia katika uigizaji. Kwa mfano, muigizaji anayepewa nafasi ya ulinzi, ni jambo lisiloingia akilini kwamba walinzi ni watu wenye vituko na utani mwingi wawapo kazini kama tunavyooneshwa kwenye filamu zetu.

Ni kuipotosha jamii kwani hata mtoto anajua kwamba mlinzi anapaswa kuwa makini na shujaa ili aweze kulinda na kupambana na uhalifu .

Ni wakati wa wasanii wa filamu kuwa makini katika kile wanachotaka jamii wajifunze kupitia wao kwani ni kazi yao kuielimisha jamii na sio kuipotosha jamii. Pia ni muda wa wasanii kujipanga na kuweka mikakati thabiti katika kuboresha  tasnia hii ya filamu nchini na kuigiza kulingana na maadili ya nchi yetu sio tuige kila kitu  kwa waigizaji wa nchi zingine.
Maudhui na fani ya filamu yeyote yanaleta msisimko pale waigizaji wanavyoigiza sawia na kufanana na hali halisi..
Nayo jamii na serikali inabidi isaidiane na wasaniii  wa tasnia hii ya filamu katika kupambana na wale wanaojinufaisha kupitia kazi zao. Kama kulalamika, wamelalamika sana hasa kwa watu “wacable”

Serikali inashauriwa kuweka mkazo kwenye  sheria za hakimiliki za wasanii na pia faini iongezwe ili iwe ngumu kwa mtu kulipa pale anapopatikana na kosa la kusambaza kazi za wasanii bila idhini ya wasanii hao.

Thursday, January 27, 2011

Askofu Mdegella kujenga Msikiti

Na Abela Msikula

ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) dayosis ya Iringa, Dk. Owdernburg Mdegella ameahidi kuwajengea msikiti wanajumuiya ya kiislam wa Chuo Kikuu cha Tumaini Iringa ili kuwapunguzia adha ya kukosa mahali jirani pa kufanyia ibada.

Askofu Dk. Mdegella ambaye pia ni Mwenyekiti wa bodi ya Chuo hicho alitoa ahadi hiyo hivi karibuni wakati wa sherehe za kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza chuoni hapo.

“Nitasimamia mwenyewe ujenzi kuanzia hatua ya mwanzo hadi mwisho” alisisitiza Askofu Mdegella katika sherehe ambazo pia zilihudhuriwa na Mbunge wa Jimbo la Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Alisema hapendi kuona wanafunzi wa kiislamu chuoni hapo wakikosa mahala maalum pa kufanya ibada zao, hivyo atahakikisha anatafuta eneo jirani na chuo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hiyo ya ibada.

Akitoa maoni yake kufuatia ahadi hiyo, Kiongozi wa jumuiya ya wanafunzi wa kiislam chuoni hapo, Alli Ng’omberaye alisema watafarijika kama ahadi hiyo itatekelezwa kwani mara nyingi ni mara chache kuona ahada za majukwaani zikitekelezwa.

Kama hilo lingekua katika utekelezaji wa haraka kama Askofu alivyotamka, tayari jumuiya ingekuwa na taarifa maana sisi ndio wahusika hawezi kufanya kitu kama hicho bila kutuhusisha” alieleza shaka yake Ng’omberaye.

Naye mchungaji Betson Sevetu ambaye ni Mshauri wa kiroho wa usharika wa chuoni hapo alisema kwa uwezo wa Askofu hilo linawezekana lakini anafikiri linaweza kuchukua muda mrefu kukamilika kwani kuna jukumu la muda mrefu la ujenzi wa kanisa chuoni hapo ambalo halijakamilika.

“Hata sisi tuna eneo tulilotengewa kwa ajili ya ujenzi
wa kanisa hapa chuoni yapata miaka saba iliyopita lakini hadi leo hata shughuli za ujenzi hazijaanza “. alisema Mchungaji Sevetu.

Baadhi ya wanafunzi waliozungumza na mwandishi wamesema hatua hiyo ya Askofu Dk. Mdegella kama itatekelezwa itakuwa ya kihistoria na chachu ya kuimarisha mahusiano ya watanzania bila kujali imani za kidini.

Chuo Kikuu cha Tumaini Iringa kinamilikiwa na KKKT dayosisi ya Iringa. Hata hivyo kinadahili wanafunzi katika kozi  mbalimbali bila kujali dini.

Monday, January 24, 2011

Dk. Mdegella amjibu Chatanda, Makamba

    Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri dayosisi ya Iringa,
    Dr. Owdenburg Moses Mdegela

Na Elisha Magolanga, IUCo                                                    
ASKOFU wa Kanisa la Kiinjiri la Kilutheli Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa, Dk. Owdenburg Mdegella amesema kamwe Maaskofu hawataacha kutolea maoni masuala ya kisiasa  kwani kufanya hivyo ni sawa na kujitenga na masuala nyeti yanayohusu jamii.

“Siasa ndiyo maji, shule, barabara, umeme, na matibabu ya waumini wetu.... alisema Dk. Mdegella wakati akihutubia sherehe ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Tumaini Iringa mwishoni mwa wiki.

 Askofu Mdegella alikuwa akijibu kauli za Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Marry Chatanda na Katibu Mkuu wa CCM taifa, Yusuph Makamba ya kutaka Maaskofu kuvua majohoo iwapo wanataka kujihusisha katika siasa.

Askofu Mdegella ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho alisema kinachowasibu wanasiasa wengi hapa nchini ni kutokuwa na elimu ya kutosha hivyo kushindwa kujenga hoja za maana na  zenye manufaa kwa jamii. 

“Serikali ya Tanzania itegemee kupata changamoto kutoka kizazi hiki kwani wanapozalisha wasomi wategemee pia kupata changamoto...hii ni sawa na kuwasha moto na kisha kuuweka chini ya kiti walichokikalia hivyo wategemee kuungua” alieleza Askofu huyo katika sherehe ambazo pia zilihudhuriwa na Mbunge wa jimbo la Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Alisema wasomi wana jukumu la kuwa kioo na mbegu njema katika jamii wanazotoka kwa kuibadilisha jamii ili iwe na viongozi wenye hofu ya Mungu ili kuepusha tatizo la kuwa na uchafu wa Dowans, EPA, Richmond, Meremeta na Loliondo.

Hivi karibuni Chitanda alitoa kauli ya kuwapinga maaskofu na kuungwa mkono na Makamba  baada ya maaskofu wa Mkoa wa Arusha kutoa tamko la kutokumtambua Meya wa Manispaa ya hiyo,  Gaudence Lyimo na kuahidi kutompa ushirikiano kwa madai kwamba Serikali ya CCM ilihujumu mchakato wa uchaguzi wa Meya huyo.

Maaskofu walilaani kitendo cha polisi mkoani huo kutumia nguvu kubwa kuliko kawaida katika kuzuia maandamano hayo, na matokeo yake watu watatu walikufa na wengine zaidi ya ishirini kujeruhiwa kwa risasi za moto.

Katika hatua nyingine, Askofu Dk. Mdegella alimtaka Mbunge Msigwa  kufikisha bungeni kilio cha wanafunzi juu ya urasimu wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu hapa nchini ambao unadhoofisha ubora wa elimu.

“Nakuagiza, lichukulie suala la mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa uzito mkubwa, tunataka kila mwanafunzi anayedahiliwa kuingia Chuo Kikuu apate mkopo bila kujali ni maskini au tajiri, daraja la kwanza au la tatu... kama tatizo ni fedha watuambie sisi wananchi ndio wenye mamlaka ya kulitatua suala hilo” Alisema.

Naye Mchungaji Msigwa aliwataka wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kukataa kutumiwa vibaya na wanasiasa wanaolenga  kujinufaisha wenyewe na kuweka pembeni maslahi ya taifa.

Alisema ni vyema wasomi wakatumia fulsa walizonazo kama nyenzo ya kulikomboa taifa kutoka katika ujinga na umaskini kwa kuwajibika kuelimisha umma masuala yanayohusu mustakabali wa kukuza uchumi wa taifa.