Wednesday, April 13, 2011

Mzee Pwagu:Injinia wa umeme Njombe asiyefahamika

Kuna watu wengi wanaoweza kuisaidia serikali kutatua tatizo la umeme kama watatumika ipasavyo.
Bahati mbaya serikali yetu inashindwa kuwatupia macho na kuwaacha waende na vipaji vyao, 
huku taifa likizama katika giza. Mmoja wa watu wenye uwezo wa kuzalisha umeme John Mwafute,mwenye umri wa miaka 81anayefahamika zaidi kwa jina la Mzee Pwagu kutoka mjini Njombe.
Mzee Pwaguaada ya kumaliza elimu yake ya msingi alijifunza kazi ya uhunzi, kidogo kidogo akaanza kujifunza na mambo ya umeme. Alipopata ujuzi katika uhunzi na umeme, akaanza kubuni vifaa mbali mbali ambavyo vilikuwa vinamsaidia katika kazi zake za uzalishaji umeme wa maji.
Alianza kwa kuzalisha umeme wa kilowatt 1.
Baada ya kuona juhudi zake na uwezo wake wa kuzalisha umeme, akapata mafunzo zaidi kutoka kwa Godfrey Ndeo kwenye mambo ya uinjinia.
Hivi sasa anazalisha umeme wa" phase 3" ambao una uwezo wa kuendesha kiwanda, lakini anautumia katika karakana yake iliyopo Mji mwema, nje kidogo ya mji wa njombe.
Mzee Pwagu, ameamua kuwafundisha vijana juu ya ujuzi alionao. Kwa kuanza ameanza navijana walio kijiji cha Chamani, kilometa Kumi na tano kutoka njombe mjini.
Lengo lake ni kuwafikishia umeme watu wa vijijini na sehemu zote ambazo serikali imezisahau, katika huduma ya umeme.
Mafunzo kwa vijana wa kijiji cha chamani yamechukua muda wa mwaka mmoja hadi kukamilika na hivi sasa nao wanafurahia umeme uliozalishwa nao kwa msaada wa mzee Pwagu
Mzee Pwagu ni changamoto kubwa kwa "Dowans" na serikali kuhusiana na suala zima la tatizo la umeme. 

Mzee Pwagu      






"Ngoja nikuonyeshe kijana"

"Umeona mambo yangu ?Hili trela tu picha linakuja"Mzee Pwagu akimuuliza Raphael Nyoni, mwanahabari toka chuo kikuu cha Tumaini,Iringa

Hapa anasema "haya sasa twende nikupeleke kwenye power station"

No comments:

Post a Comment